Thursday, October 23, 2008

Nani anayestahili kuwa msanii na kuchambua kazi za wasanii?

Ingekuwa watanzania wengi wanaelewa maana ya sanaa ni wazi kuwa sanaa yetu ya Tanzania ingekuwa katika kiwango cha kimataifa. Ni dhahiri mtu atajiuliza kuwa, mbona filamu nyingi za kitanzania zinatungwa na idadi ya wasanii hususan wa muziki huongezeka kila uchao wa jua lakini eti mimi nasema watanzania wengi hawaelewi ni nini sanaa?.

Ni rahisi kuwasikia wasanii wenyewe wakijipongeza kutokana na kasi ya ukuaji wa sanaa huku na jamii nayo ikiwa na matumaini kuwa sasa Tanzania inaingia katika soko la kimataifa katika sanaa. Lakini husahau kuwa ongezeko la wasanii halimaanishi kuwa sanaa ya bongo inakua na badala yake wimbi kubwa la ongezeko la wasanii wetu linachangia kuporomoka kwa fani hii kitaalamu.

Wengi huiona sanaa kama ni kazi rahisi kuliko kazi zote ulimwenguni na mtu yoyote anaweza kuwa msanii au jaji wa kazi za sanaa. Kwa Tanzania mtu yeyote mwenye pesa anaweza kutengeneza kitu kinachoitwa filamu au kuwa producer kwa kuanzisha studio binafsi. Hili ni kosa kubwa ambalo linarudisha nyuma maendeleo ya sanaa hapa nchini.

Tofauti na nchi zilizoendelea ambapo wao huiona sanaa kama ni taaluma na kumuona msanii kama ni mtu mwenye taaluma na kipaji Fulani, ndio maana wao Huiheshimu kazi hiyo, na huamini kuwa ili mtu aitwe msanii lazima awe na ujuzi alioupata kutokana na kile alichosomea mbali na kipaji. Hali hii hufanya kazi za wasanii wa nje kuonekana ni bora na kukaa kwenye chati muda mrefu kuliko kazi za wasanii wetu.

Kwanza kabisa wasanii wetu wengi hawana elimu juu ya kile wanachokizalisha. Waigizaji wengi wa Tanzania huokotwa, yaani mtu yeyote mwenye pesa anapotaka kutengeneza filamu hutafuta watu ambao yeye anaona kuwa wanaweza kuigiza na sio kuwa wana ujuzi au uzoefu wa kucheza filamu, na mtu huyo mwenye pesa yeye huwa kama director.

Kinachofanyika hapa ni uwezo wa kipesa ndio unaompa kiburi na sio utaalam. Sasa huyo director mwenyewe hana utaalam matokeo yake kinachoonekana kwenye filamu hiyo ni dhahiri kabisa kuwa utaona watu wakiigiza kwa vile wamekariri maneno na sio wameelewa wanaigiza kitu gani.mfano hebu angalia filamu hizi “usikose kwenye mazishi yangu na Laheri” waigizaji wake wote nawamekariri maneno hali inayomboa mtazamaji kwani haimpi msisimko mtazamaji wa filamu hizi, tofauti na unapongalia filamu za nje kama vile “remember your mother”, “Prison break” na nyinginezo nyingi.

Uhalisia wa maisha ya kitanzania hauonekani katika filamu nyingi za kibongo. Wengi wa wanaotengeneza filamu huiga uhalisia wa maisha ya ughaibini au ya kinigeria. Wengi huonesha maisha ambayo watanzania hawaishi.

Hata wasanii wetu wanapoamua kuigiza juu ya tamaduni za kitanzania basi mara nyingi sana hutumia tamaduni za kinigeria kuanzia mavazi hadi destuei ni za kinigeria. Mnigeria anapoangalia filamu hizi moja kwa moja atajua ni jamii yake ndiyo inayozungumziwa. Hivi ina maana watanzania hatuna utamaduni wa makabila yetu licha ya kuwepo makabila zaidi ya 100 hapa nchini?.

Hawa waigizaji kutuletea maisha ya kigeni kuanzia mavazi hadi utamaduni, kitu ambacho hukikuti katika jamii zetu ina maana wao hawajui hali halisi ya Tanzania, wanavyoishi watanzania, na changamotop zinazowakabili?.

Kipi ambacho katika filamu zetu za bongo mkulima anayetumia jembe la mkono, mpiga debe na mmachinga anaweza kunufaika nacho?. Filamu hizi zitaibua lini masikio ya mafisadi? Zitaibua lini jamii ambazo bado zina mila zisizofaa kama ukeketaji, Zitamuibua lini mlalahoi anayeishi chini ya dola moja kwa siku na kumsaidia?

Hatuoni wakiigiza jinsi wakulima wanavyopata tabu katika kilimo na hata katika uuzaji (soko), jinsi wamachinga wanavyopigwa kila siku na wanamigambo na jinsi ndugu zetu wakulima na wafugaji wanaopigana kila siku kwa sababu ya ardhi.

Ni mambo mengi ambayo yangewezwa kutengenezewa filamu Tanzania ili kuwaelimisha watanzania na kuwaburudisha kulingana na kuwa na uhalisia zaidi wa kitanzania na sio wa kigeni.

Soko huria nalo linaharibu fani hii kwani kuwepo na uhuru wa mtu yeyote kutengeneza filamu au kuwa producer, jaji na hata msanii bila kuangaliwa kama ana vigezo au la kumetuletea mambo yote haya ya kuvuruga sanaa. Kwani hakuna chombo chochote kinachohakiki kazi ya sanaa kabla ya kuingia sokoni.

Endapo kazi hizi zingekuwa zinafanyiwa utafiti na kusajiliwa na wataalam waliobobea katika fani hii tusingeona kazi zisizokuwa na mwelekeo na wasanii wangekuwa wachache na wanaheshimika. BASATA ina jukumu kubwa la kuifufua hadhi ya sanaa hapa nchini kwa kufuata mawazo haya.

Ningependa hadhi ya sanaa irudishwe nchini, tuna wasomi wengi chuo kikuu cha Dar es salaam katika idara ya sanaa na vyuo vingine vya sanaa hapa nchini, nadhani wanajukumu la kuikomboa sanaa ya Tanzania kama kweli wataweka nia ya dhati ya kuikomboa fani hii wanayoisomea kwa muda mrefu.

Huwa kila siku najiuliza mbona kila mwaka UDSM inatoa wataalamu wa sanaa lakini kinachofa nyika ni mauaji ya fanii hii na sio maendeleo? Wataalamu wetu wanaenda wapi au ndio wanakimbilia nje kwa ajili ya maslahi? Hapana wasifanye hivyo lazima waungane waketi na kisha watafakari wataiinua vipi sanaa ya Tanzania kwani kukimbia nchi sio suluhisho. Wote tukikimbia nani atabaki kuwa mtanzania mzalendo na kuikomboa sanaa hii?

Tukirudi katika muziki hususan Bongo Flava mambo ni yaleyale. Tatizo la elimu bado linajitokeza miongoni mwa wasanii wengi. Nikisema elimu simaanishi kuzungumza kiingereza, maana siku hizi wasanii wanaona ili kutoa kale kanakoitwa ujinga na kuonekana mjanja na msomi ni kujua kiingereza na sasa wasanii wengi wanazungumza lugha hii hata zaidi ya wasomi, tena sifa eti hata wanapohojiwa hujidai kuwa hawafahamu Kiswahili vizuri kwa kuchanganya na msamiati wa kiingereza.

La hasha! Mimi namaanisha elimu juu ya muziki. Ukiangalia kwa umakini na kwa undani zaidi wasanii wa bongo nao ni kama waigizaji wa filamu, wengi huimba muziki kwakuwa wana pesa au studio. Lakini vilevile wengi hujiunga na muziki baada ya kushindwa maisha. Yaani wengine hushindwa shule au kujikwamua kimaisha kutoka katika dimbwi la umasikini kwa kutumia njia nyingine na kuamua kuingia katika fani ya muziki.

Hapa wengi wao huuona muziki kama vile ni kitendo cha kuimba. Hawajui hata historia ya muziki mambo yaliyomo katika muziki na katika dunia ya leo ya utandawazi msanii anawezaje kukaa katika chati na kupata tuzo za kimataifa ndio maana nyimbo nyingi za bongo hupanda na kushuka chati haraka tofauti na miziki ya wenzetu.

Kwa haraka haraka kama ni mfuatiliaji mdogo wa muziki kama mimi, juzijuzi tu wimbo wa matonya uitwao “Anita” ulikuwa katika chati na ulikuwa unasikika karibu kila baada ya dakika 15 katika vituo mbalimbali vya radio na TV hapa nchini lakini leo hii hata siku tano zinapita bila kuusikia na ndio hata mwaka haujaisha na hata unapopigwa tena watu wanasikiliza lakini si kwa hamasa kama hapo awali.

Hata unapoangalia kumi bora katika za EATV kama kituo cha television kinachohusu burudani zaidi nyimbo nyingi zilizomo kwenye chati ni za ughaibuni. Hebu tutumie mfano huu pasi na kuangalia wanaopanga kumi bora hizo kama wana uelewa na fani ya muziki au la! Hata kama hawana uelewa kwanini nyimbo nyingi zinazoshika chati ziwe za ughaibuni na sio za bongo na kwanini nyimbo za bongo zishuke chati haraka tofauti na za huko magharibi? Tatizo ni nini na ile hali wote ni wasanii?

Hapa tatizo bado ni lilelile, watu hawaheshimu kazi za watu na ndio maana watu wengi wanaghushi kazi za wasanii na hupita barabarani bila wasi ni kwakuwa anayefenya kazi ya muziki anachotaka ni pesa ya kula mengine hajali, na akishanunua gari na kujenga kijumba kimoja anaona kashinda maisha na ni msanii bora kumbe anatakiwa aipandishe heshima kazi yake, kwake yeye akishapata ni sawa na waswahili wasemavyo “masikini akipata matako hulia mbwata”.

Sisemi hivi eti kwa kuwafagila wanaoghushi kazi za wasanii ila ni kwa kuwahurumia wasanii kwani huko tunakoeleka ni kugumu zaidi kama wasanii hawawatataka kujiona wasanii, kuthamini kazi zao na kuziwekea heshima basi jamii haitaziheshimu na badala yake kila siku wasanii wataishia kulia.

Sasa umefika wakati kwa Tanzania kuheshimu na kuthamini taaluma za watu si kila fani ionekane ni uzushi. Tunajua wazi kuwa japo sanaa inahitaji elimu lakini pia ni kipaji sasa sio wote tuna vipaji na hao wenye vipaji waviboreshe kwa elimu ili na sisi walau hata siku moja tuchukue tuzo ya muziki au filamu bora duniani.

Ili kuwasaidia wasanii hata waendeshaji wa vipindi vya muziki na sanaa kwa ujumla redioni na kwenye TV lazima wawe na ujuzi kwani na wao wanachangia sana kuporomoka kwa taaluma na fani hii nchini. Utakuta mtu eti kwakuwa ni mtangazaji basi hata ujaji wa sanaa anauweza. Tatizo si kujua kuongea na ujanja wa mjini matokeo yake utakuta msanii anasifiwa pasi na sifa.

Na pia waandaji wa tuzo za muziki au filamu nao wanatakiwa wawe ni wenye kuwa na ujuzi juu ya taaluma au fani hiii muhimu duniani.

Ni vema wasomi nao wakatia nguvu hili. Na endapo kutakuwa na bodi ya kuhakiki kazi za wasanii ni wazi kuwa hata hao wanaojiita maprodyuza ambao hawana ujuzi hawatakuwepo na watasoma na sasa sanaa yetu ya Tanzania itakuwa na sura mpya ulimwenguni.

HUU UCHAFU BONGO

Licha ya msongamano wa watu na foleni za magari bado ipo sifa moja kubwa ya uchafu katika jiji la Dar es salaam. Ni sifa ambayo wengi wetu huisahau katika wasifu wa jiji hili la Dar es salaam, lakini pindi unaposhuka ubungo kutoka mikoa mingine au nchi jirani ni lazima uso wako utakutana na uchafu mwingi unaotabasamu huku ukikukaribisha kwa mbwembwe ukisema “karibu mgeni”.

Ingawa kwa kiwango fulani serikali inajitahidi kuliweka jiji katika hali ya usafi ikiwa ni pamoja na kuweka mabango sehemu mbalimbali za jiji yakiwa na ujumbe wa “weka jiji safi” na kuweka ndoo maalum kwa ajili ya kuwekea uchafu sehemu mbalimbali za jiji ili kuimarisha usafi na hata baadhi ya daladala kuwa na ndoo hizo lakini bado haijafanikiwa kwa kiwango cha kuridhisha, kutokana na uchafu kuzidi kutapakaa kila kona ya jiji na mlipuko wa magonjwa yatokanayo na uchafu ukiwemo ugonjwa wa kipindupindu ambao hushambulia kwa kasi jiji hili kila mwaka kasi ambayo naweza sema kuwa ni kubwa ukilinganisha na mikoa mingine.

Harufu mbaya hutawala maeneo mengi ya jiji kutokana na uchafu, hususan kipindi cha mvua ambapo wakazi wengi wa jijini hufungulia maji machafu ya chooni ili kukwepa gharama za unyonyaji wa maji hayo, jambo ambalo huhatarisha afya na pia ni kero kwa wapita njia na wakazi jirani wa maeneo hayo.

Tatizo bado ni kubwa na mbaya zaidi uchafu huo huzagaa hadi maeneo ya posta ambapo ofisi kubwa za serikali zipo maeneo hayo zikiwemo wizara nyeti hapa nchini.

Imekuwa ni kitu cha kawaida kukutana na uchafu katika sehemu za soko na hata katika migahawa mbalimbali ya jijini ambapo mara nyingi mteja hukaribishwa kwa nderemo na vifijo vya wadudu inzi. Ni jambo la aibu sana kwa watanzania lakini limeshazoeleka na kuonekana kama ni sehemu muhimu ya maisha ya jijini.

Japokuwa watanzania hawana desturi ya usafi lakini umasikini nao unachangia kuongezeka kwa uchafu jijini. Kutokuwepo kwa vyoo vya umma vinavyotoa huduma bure kunasababisha ongezeko la uchafu.

Serikali inapiga kelele juu ya uchafu lakini inasahau kuwa si watanzania wote wenye uwezo wa kumudu gharama za choo. Kwa muuza maji, mpiga debe na watu wengi wasio na ajira kamwe hawataweza kulipia sh 100 kwa ajili ya kwenda msalani kujisaidia.

Ikiwa mtu anapata sh 500 kwa siku pesa ambayo haitoshi hata mlo wa siku moja ni wazi kuwa mtu huyo anapotaka kwenda msalani atapita uchochoroni na kufanya mambo yake. Ndiyo maana unapopita katikati ya jiji harufu ya mikojo na kinyesi ni jambo la kawaida kwa wakazi wa jijini. Kama serikali haitajenga vyoo vya umma sura mpya ya usafi katika jiji hili itakuwa ni ndoto.

Mamlaka ya maji safi na maji taka ina huduma ambazo zimelenga kwa watu wa hali ya juu, daima mwananchi wa kawaida hatoweza kunufaika na huduma hizi kutokana na gharama kubwa za utumiaji.

Harufu mbaya waipatayo wananchi hawa kutokana na kufungulia maji machafu ya chooni ili yasafirishwe na mvua, haiwafurahishi na kila mara serikali hukemea tatizo hili. Lakini ukemeaji wake hubaki kuwa wa mdomoni usiokuwa na utendaji.

Huduma nyingi za utoaji wa maji taka katika jiji la Dar es salaam hugharimu kati ya sh 25,000 hadi 70.000. ni watanzania wangapi wenye uwezo wa kumudu gharama hizo? Serikali au mamlaka husika imeweka mkakati gani ili kuwasaidia watu wa kipato cha chini ambao hupata chini ya dola moja kwa siku?

Kama huduma hii ingetolewa bure au kwa kiwango cha kumfanya kila mtanzania hasa yule anayeishi chini ya dola moja kwa siku aweze kumudu gharama hakuna mtu ambaye angefungulia maji hayo ili apate upepo wa kinyesi na kuhatarisha afya yake.

Kwa mamlaka ya maji safi na maji taka kuweka eneo la maji taka karibu na makazi ya watu maeneo ya buguruni kunamaanisha kuwa hata wahusika wa usimamizi wa mradi huu hawana uelewa juu ya usafi wa mazingira. Japokuwa walidai kuwa eneo hilo liliwekwa kabla ya watu hawajaweka makazi maeneo hayo lakini ilipaswa kutambua juu ya umuhimu wa afya na mazingira na sio kuwatupia lawama wananchi kwa kujenga makazi yao karibu na maji taka. Jukumu lao ni kuwasaidia wananchi na pengine kuihamasisha serikali ili wananchi hao waweze kuhama mahali hapo na kuwaelimisha wakazi hao.


Halmashauri husika za jijini zimezuia ubebaji hovyo wa taka ambapo baadhi ya watu hususan vijana hujiajiri kwa kupita majumbani mwa watu na kubeba taka na kisha huenda kuzitupa sehemu isiyo rasmi jambo ambalo ni kero kwa wengi kwani mara nyingi husubiri nyakati za usiku na kuzitupa taka hovyo katika misingi ya barabarani, nyumba za ibada na hata majumbani mwa watu. Utekelezaji wa jambo hili bado haujafanikiwa kwani serikali imekataza bila kuweka njia mbadala.

Licha ya kuwepo kwa magari maalum ya kubeba taka lakini kumekuwa na usumbufu mkubwa sana katika huduma hiyo. Kwanza magari ni machache na hayapiti pembe zote za jijini isitoshe hayana ratiba maalum, kwani unaweza kukaa miezi miwili bila kuliona gari hilo likipita kuchukua uchafu. Hii inapelekea ugumu kwa wakazi kuvumilia uchafu wenye harufu kali ndani ya mwezi mzima na ndio maana wengi hutumia njia zisizofaa ili kuweka nyumba zao katika hali ya usafi.

Hivi hizi ratiba hewa za haya magari huwa ni sehemu zote za jiji hata Masaki na Osterbay au ni kwetu tu mwananyamala kwa walalahoi? Ina maana hata viongozi nao hukaa na uchafu kwa muda usiojulikana? Kama mwendo ndio huo ni vema kwani naamini kuwa viongozi nao watakuwa wanatumia shortcut kutupa taka zao na wanajua fika kuwa hata iweje jiji haliwezi kuwa safi.

Kwa upande wa elimu inayotolewa kila mara na serikali na mashirika binafsi bado haijafaulu kwani elimu hii imekuwa ikitolewa bila kuangalia chanzo halisi cha uchafu wa jijini. Tatizo si msongamano wa watu pekee tatizo ni miundombinu mibovu, ufuatiliaji mbovu wa sera na umasikini, na umasikini ni sababu kuu mojawapo lawama zisitupwe tu kwa wananchi bila kuisahau serikali. Hata ukiwaambia watanzania waache kutupa taka hovyo je, serikali imewawezesha katika nyanja zote? Sio kuwaambia waache kutupa taka hovyo bila kuwawekea njia mbadala.

Hata hivyo elimu kwa wananchi pekee haitasaidia bali hata viongozi nao waelimishwe kwani tabia ya kutuletea magari yanayopita mara moja baada ya miezi tumeichoka na kama ratiba hizi ni kona zote za jiji hadi wanakoishi viongozi wetu ni wazi kuwa na viongozi wetu nao hawana elimu ya kutosha juu ya usafi. Inatakiwa sisi na viongozi tujifunze kuthamini chakula na yale yatokanayo na chakula ili kuimarisha usafi.

Kutokana na mfumo mpya wa serikali wa kuunda tume ili kuchunguza mambo mbalimbali naona sasa kuna umuhimu wa serikali yetu kuunda tume ili kuchunguza chanzo cha uchafu jijini labda hali ya usafi wa jiji hili unaweza kuimarika muda wote na sio kipindi cha akina Bush na wageni maarufu wanapotaka kuja nchini.

Sunday, October 12, 2008

Hotel Menu Ya Kikamba kule Bungoma,Kenya


Tonut na maantasi 5.00 /=
Homelet Plain 4.50/=

Jai na zgonji 5.00/=
Tenku na ukali 6.00/=

Jabati Pantika 6.40/=

jabati na karanka 15.00/=

Gugu ya ingo 50.00/=
Gugu ya genjik 25.00/=

Mgade Poflo 6.50/=

mapawa ya ingokho(chumusha)10.00 pop

mapawa ya ingokho( choma) 15.00 pop

Zdrungi kafu 1.50/=

Matonto na Mihoko 30.00/=

Zamagi ntoko 23.00/=

Enchoy your meals

bay at te counder

The Most Pierced Woman



WHO:
Elaine Davidson
WHAT:
720 piercings
WHERE:
Edinburgh, Scotland, UK
WHEN:
August 9, 2001

By August 9, 2001, Elaine Davidson, of Edinburgh, Scotland, had a record-breaking total of 720 piercings. She first broke the record in May 2000, when a Guinness World Records official examined her and found 462 piercings on various parts of her body, including 192 on her facial area alone

The longest Hair



WHO:
Xie Qiuping
WHAT:
5.627 m (18 ft 5.54 in)
WHERE:
Guangxi Province, China
WHEN:
May 8, 2004

The world's longest documented hair belongs to Xie Qiuping (China) at 5.627 m (18 ft 5.54 in) when measured on May 8, 2004. She has been growing her hair since 1973 from the age of 13.

Saturday, October 11, 2008

The Smallest waist in The World




Cathie Jung
WHAT:
38.1 cm (15 in)
WHERE:
Old Mystic, Connecticut, USA
AGE:
72

Cathie Jung's waist is about the same size as a regular jar of mayonnaise. She's been wearing a corset every day for the past 12 years, and she now wears one 24 hours a day. "I probably have around 100 of them," says the corset queen.

The Heavy Hammer


A group of prisoners are on a manual work at kurasini were filling a foundation trench ready for concrete casting. One prisoner who has been assigned a particularly tough job of breaking huge stone to reduce them into smaller sizes using a-5kilo hammer before laying them decides to have a break.
The supervisor is up on him almost immediately and orders him back to work. "Give me a break", the prisoner complains, "Don't you reliase this hammer is heavy?"
"So, the hammer is heavy now?" Says the supervisor; "But when you were stealing the freezer you managed to run with it on your back!from Afrika sana to Sinza kwa Remy,so there is no reason for you to start complaining Now get back to work"

A Very Depressed Man


There's a man sitting at a bar just looking at his drink. He stays like that for half an hour. Then, a big trouble-making truck driver steps next to him, takes the drink from the guy, and just drinks it all down.

The poor man starts crying. The truck driver says, "Come on man, I was just joking. Here, I'll buy you another drink. I just can't stand seeing a man crying."

"No, it's not that. This day is the worst of my life. First, I fall asleep, and I'm late to my office. My boss, in an outrage, fires me. When I leave the building to my car, I found out it was stolen. The police say they can do nothing. I get a cab to return home and when I leave it, I remember I left my wallet and credit cards there. The cab driver just drives away. I go home and when I get there, I find my wife sleeping with the gardener. I leave home and come to this bar. And when I was thinking about putting an end to my life, you show up and drink my poison."

Thursday, October 9, 2008

Learning To Like Yourself


Today I would like to talk about learning to like yourself,you and I have to learn to deal with our "do" separately from our "who"? The fact is, no one does everything right all the time, but that doesn’t affect who I am. We have made mistakes in our lives and I’m sure we'll still make mistakes in the future—but we still must like ourselves.

If you like yourself—even though others may not—you’ll make it. When you start to like yourself, other people begin to like you too. Liking yourself doesn’t mean you’re full of pride; it simply means you accept yourself as the person God created you to be. We all need changes in our behavior, but accepting ourselves as God’s creation is vital to our progress in becoming an emotionally healthy person. If we can master this one thing—liking ourselves—it will work wonders in helping us to overcome a shame-based nature. OK maybe let me explain what I mean.

Many people live under what I can call the curse of failure. They can never do anything they set out to do. They’re always failing, always messing up, always getting disappointed, discouraged and depressed. They don’t like who they are because they’ve adopted a shame-based nature.

For a long time I didn’t like my personality, and since my personality is who I am, I didn’t like me. I didn’t want to be as bold and straightforward as I am. I didn’t want to be so direct and blunt. I wanted to be like one of my friends. She had a gift of being sweet, kind and gentle. What I didn’t realize is that she was just born that way—and I wasn’t. Because I didn’t like my personality and who I was, I tried to change myself. I wanted to be more like my friend. I tried to be the perfect girl but I always upset or disappoint the ones I love especially my mum.

It didn’t work. I was just trying to be something I wasn’t. Finally, I had to learn to accept myself the way I was and let go of the idea of being like someone else. I began to realize that, although I did need to change some areas of my life, who I am will never change.

For example, those are physically abuse,being called funny names or being verbally insulted is a very destructive disorder in Bongo today. These kind of people who are distructed can never enjoy their lives.

Workaholics,emotionally destroyed and physically abused are examples of the types of people who really haven’t learned to simply like who they are. Shame, because of something they may have happened or done in their past, has caused them to dislike themselves. Remember, you must separate your "do" from your "who". You’re a unique and special individual, with God-given talents and skills. And even though you may have made mistakes in the past, it’s time to move on and learn to like yourself!

The Stairs


Bill, Jim, and Scott were at a convention together and were
sharing a large hotel room on the top of a 75 story building.
After a long day of meetings they were shocked to hear that the
elevators in their hotel were broken and they would have to climb
75 flights of stairs to get to their room. Bill said to Jim and
Scott, let's break the monotony of this unpleasant task by
concentrating on something interesting. I'll tell jokes for 25
flights, and Jim can sing songs for 25 flights, and Scott can
tell sad stories the rest of the way. At the 26th floor Bill
stopped telling jokes and Jim began to sing. At the 51st floor
Jim stopped singing and Scott began to tell sad stories. "I will
tell my saddest story first," he said. "I left the room key in
the car.

THE PRESCRIPTION...

A nice, calm and respectable lady went into the pharmacy, walked right
up to the pharmacist, looked straight into his eyes, and said, "I would
like to buy some cyanide."

The pharmacist asked, "Why in the world do you need cyanide?"

The lady replied, "I need it to poison my husband."

The pharmacist's eyes got big and he exclaimed, "Lord have mercy!

I can't give you cyanide to kill your husband! That's against the law!
I'll lose my license! They'll throw both of us in jail! All kinds of bad
things will happen. Absolutely not! You CANNOT have any cyanide!"

The lady reached into her purse and pulled out a picture of her husband
in bed with the pharmacist's wife.


The pharmacist looked at the picture and replied, "Well now, that's
different. You didn't tell me you
had a prescription."